Followers

logo logo

SLIDE

[10] [recent] [slider-top-big] [HABARI KALI ZA WIKI]
[4] [NEWZ] [slider-top] [Habari]
You are here: Home / SOUDY BROWN KURUDISHWA MAABUSU

SOUDY BROWN KURUDISHWA MAABUSU

| No comment

Kesi inayomkabili mtangazaji wa Clouds Media Soudy Brown, leo imesikilizwa katika Mahakama ya Hakimu Mkazi Kisutu, upande wa utetezi ukiwakilishwa na Wakili Peter Kibatala akisaidiana na Wakili Maghimbi.

Image result for SOUDY BROWN

Katika maelezo ya awali Soudy Brown anashtakiwa kwa kosa la kurusha maudhui kupitia akaunti yenye jina la Shilawadu ambayo haijasajiliwa 


Baada ya Hakimu kusikiliza kesi hiyo upande wa utetezi umeomba mshtakiwa apewe dhamana ambapo Hakimu amekubali hivyo mshtakiwa ametakiwa kuwa na mdhamini mmoja na bondi ya shilingi milioni 2, kesi hiyo imeahirishwa hadi Octoba 18, 2018.


Hata hivyo, Soudy Brown bado anashikiliwa na amerudishwa tena  polisi  Central kwa kuwa ana kesi nyingine ya kujibu inayomhusu yeye pamoja na Msanii Maua Sama ambaye hakuletwa mahakamani leo.