Followers

logo logo

SLIDE

[10] [recent] [slider-top-big] [HABARI KALI ZA WIKI]
[4] [NEWZ] [slider-top] [Habari]
You are here: Home / LOWASSA NA MAALIM SEIF WAKUTANA KUYAJENGA

LOWASSA NA MAALIM SEIF WAKUTANA KUYAJENGA

| No comment
Image result for lowassa na maalim seif

Siku moja baada ya aliyekuwa mwenyekiti wa CUF, Profesa Ibrahim Lipumba kuwasimanga viongozi wa Ukawa kuhusu namna walivyompokea Waziri Mkuu wa zamani, Edward Lowassa na kumteua kuwa mgombea urais, viongozi hao jana walikutana katika kikao kilichotarajiwa kujadili suala hilo.

Kikao hicho cha Ukawa kimekuja zikiwa zimepita siku nne baada ya Lowassa na Katibu Mkuu wa CUF, Maalim Seif Sharif Hamad kukutana nyumbani kwa Lowassa Jumatatu ya wiki hii.

Juzi, katika mahojiano na kituo cha redio cha Clouds FM, Profesa Lipumba alisema mkutano wa chama hicho ulioridhia Lowassa kuingia Ukawa ulifanyika Zanzibar bila yeye kuambiwa, kitendo kinachoonyesha kuwa Katibu Mkuu wa CUF, Maalim Seif Sharif Hamad alikuwa akimzunguka.

Mbali na tuhuma hizo, kiongozi huyo alieleza kuwa hatakuwa tayari kuona CUF ikinunuliwa kwa bei chee na Lowassa au Chadema hata kama atakuwa nje ya chama hicho.

Jana jioni, viongozi wa vyama hivyo walikutana faragha kwenye ofisi za Lowassa zilizopo Mikocheni. Haikuweza kufahamika mara moja ajenda za kikao hicho lakini habari kutoka ndani ya vyama hivyo zilisema pamoja na mambo mengine kilitarajia kujadili shutuma zilizotolewa na Profesa Lipumba.

Suala jingine lililotarajiwa kujadiliwa na viongozi hao washirika wa Ukawa ni mkakati wa pamoja wa namna ya kuendesha shughuli za siasa katika kipindi ambacho imetolewa amri ya kuzuia maandamano na mikutano ya siasa.