Followers

logo logo

SLIDE

[10] [recent] [slider-top-big] [HABARI KALI ZA WIKI]
[4] [NEWZ] [slider-top] [Habari]
You are here: Home / MKURUGENZI WA MKOA AZICHARUKIA BAA NA KLABU HIZI ZA USIKU …!!

MKURUGENZI WA MKOA AZICHARUKIA BAA NA KLABU HIZI ZA USIKU …!!

| No comment

SHINYANGA

MKURUGENZI Mtendaji wa Manispaa ya Shinyanga, Lewis Kalinjuna amezifunga baadhi ya kumbi za starehe na baa ya Dragoni iliyokuwa karibu na Shule ya Msingi Town kwa madai kuwa zimekosa viwango vinavyotakiwa ikiwemo kukosa huduma za vyoo.

Licha ya changamoto hiyo, katika shule hiyo ya msingi ndani ya madarasa kumekuwa mara kwa mara kukutwa na kondomu ambazo zimekwisha tumika hali ambayo ni hatari kwa wanafunzi.

 

Akizungumza na waandishi wa habari mjini hapa jana, mkurugenzi huyo alisema klabu za usiku za Bakurutu maarufu Maduka Mengi, Lubaga Inn na Butiama zimefungwa mpaka zitakapojirekebisha kwa kutengeneza huduma zinazotakiwa.

Kalinjuna alisema baa ya Dragon imefungwa moja kwa moja kutoa huduma kwa sababu ya kutokukidhi viwango hasa kukosa huduma za vyoo na kuwa karibu ya eneo la shule.

“Hizi baa za usiku zinazokesha zimekuwa na changamoto nyingi hivi sasa ni suala la usafi kila maeneo wao wanaendesha biashara hizo pasipokuwa na huduma za vyoo. Tumeamua kuchukua hatua ya kuwasimamisha wasitoe huduma mpaka pale watakapojirekebisha ila baa ya Dragon yenyewe tumeifungia moja kwa moja,” alisema.

Mkurugenzi wa baa ya Dragon, Humprey Godfrey alisema kitendo cha kufungiwa kimemsikitisha kwani wakati akianza kufanya biashara hiyo alipewa leseni kutoka manispaa na kukagua mandhari yake sasa imekuwaje leo kufungiwa moja kwa moja hilo suala hawajatenda haki.

“Mimi nimeshangazwa na manispaa hii ina maana hawakuona kipindi wanaponipatia leseni kuwa nipo karibu na shule. Sasa nimeanza biashara wamekuja kunifungia kwa kueleza makosa mengi hivyo hawajanitendea haki,” alilalama mkurugenzi huyo.