Followers

logo logo

SLIDE

[10] [recent] [slider-top-big] [HABARI KALI ZA WIKI]
[4] [NEWZ] [slider-top] [Habari]
You are here: Home / BASATA YAUFUNGIA WIMBO MPYA WA NEY WA MITEGO’SHIKA ADABU YAKO’

BASATA YAUFUNGIA WIMBO MPYA WA NEY WA MITEGO’SHIKA ADABU YAKO’

| No comment

DAR ES SALAAM


 


Baraza la Sanaa nchini(BASATA) limeufungia wimbo wa Ney wa mitego unaoitwa ‘shika adabu yako’ kutokana na matumizi ya lugha chafu ndani ya wimbo huo.

Akiongea leo na kituo maarufu cha redio, katibu mkuu mtendaji wa baraza hilo amesema ni wimbo ambao haufai na anashindwa kumpima Ney ana akili za namna gani.Image result for mtendaji basata

“Kitu ambacho hakifai kwenye jamii sio mpaka litolewe tamko kwamba wimbo umefungiwa, ni wimbo ambao haufai hata wanajamii wameona haufai, nadhani mtu mwenye akili timamu kiujumla anajua, najua kwenye media hauwezi kupigwa”

Wimbo huo mpya kutoka kwa Ney wa Mitego ulisika Live kwa mara ya kwanza kupitia kipindi cha XXL.

Katika wimbo huo uitwao ‘Shika Adabu Yako’, Ney amewaumbua kwa kuwataja majina wasanii na watu maarufu nchini akianika ubovu wa matendo yao na kuwataka wabadilike.

Pia katika wimbo amewaimba baraza la Sanaa la Taifa(BASATA) kwa kuwaita ni msumeno usiokata na kazi yao ni kufungia nyimbo ilhali hawajui shida wanayopata na kama wangekuwa watoto angewachumia fimbo.

Pia hakumuacha nyuma Magufuli na serikali yake kwa kusema amezoea wasanii ndio watu wanapenda umaarufu lakini safari hii ligi ya umaarufu ipo kwenye serikali kwa kila kiongozi kuwa na mwandishi kisha kushindana magazetini.